Ndoa, Utumwa, na Sauti za Wanawake katika Tanganyika ya Kikoloni
Ndoa, Utumwa, na Sauti za Wanawake katika Tanganyika ya Kikoloni
Dkt. Saada Omar Wahab
Wakati baadhi ya tafiti za kihistoria zimewaonyesha wanawake wa Kiafrika kama wasio na sauti
katika mijadala kuhusu utumwa na ndoa, wasilisho hili linapinga dhana hiyo kwa kutoa ushahidi
mbadala. Katika kipindi cha baada ya kukomeshwa kwa biashara ya utumwa na utumwa kisheria
katika Tanganyika ya kikoloni, mijadala kuhusu ndoa iliendelea kubeba taswira na mantiki
zinazokaribiana na zile za utumwa. Ndani ya muktadha huo, wasilisho hili linachunguza jinsi
wanawake walivyotumia uzoefu wa ndoa kueleza masuala ya mamlaka, utegemezi, na uhuru.
Uchambuzi unategemea makala zilizochapishwa kati ya miaka ya 1925 na 1926 katika gazeti la
Kiswahili Mambo Leo, hususan makala mbili za Zeina Mwinyipembe, zikionyesha jinsi wanawake
walivyojadili ndoa kwa kutumia lugha na mifano inayorejelea utumwa. Aidha, uchambuzi
unazingatia mila, matendo, na mahusiano ya kijinsia yaliyoakisi dhana za umiliki ndani ya ndoa.
Wasilisho linaonyesha ndoa kama muendelezo wa mifumo ya ukosefu wa uhuru iliyohusishwa na
historia ya utumwa.
Dkt. Saada Omar Wahab ni Mhadhiri na Mtafiti wa historia katika Chuo Kikuu cha Taifa cha
Zanzibar (SUZA). Ana Shahada ya Uzamivu katika Sayansi Jamii kutoka Chuo Kikuu cha Göttingen,
Ujerumani. Utafiti wake unajikita katika historia ya wanawake watumwa, diaspora ya Zanzibar, na
umiliki wa ardhi. Kwa sasa, anahusika na utafiti unaochunguza sauti za wanawake katika muktadha
wa utumwa na ndoa nchini Tanzania.
Kikao kitafanyika siku ya Jumatatu, tarehe 06 Julai 2026, saa kumi na robo za Ulaya ya Kati
(saa kumi na moja na robo za Afrika Mashariki) kupitia njia ya Zoom:
Veranstaltungsdetails
online